Friday, March 1, 2013

Wizi wa dawa za serikali:
KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa Tanzania (MSD) Cosmas Mwaifwani, akizungumza kwenye kongamano la kihabari lililoandaliwa na Mfuko wa Bima wa Taifa (NHIF)mkoani Mtwara alisema,"Kila mkoa kuna kesi angalau moja ya wizi wa dawa za serikali inayomkabiri mtumishi wa serikali."
Akasimulia tukio ambalo gari la MSD lilikutwa likiteremsha dawa kwenye nyumba ya mtu binafsi, tena iliyo jirani na kituo cha polisi.
Akasema hata baada ya taarifa kufikishwa kituo cha polisi, ilichukua saa tatu kwa polisi kufika, tena walikamatwa baada ya TAKUKURU kupelekewa taarifa na kuingilia kati.
"Dereva wetu aliyehusika tulimfukuza kazi lakini alirudishwa na watuhumiwa wengine mpaka leo wapo uraiani," hiyo ni kauli ya  Mwaifwani
Anasema kutokana na uzoefu alionao, kesi zote za aina hiyo serikali haishindi.
ebu toa maoni yako katika hili!

No comments:

Post a Comment