Tuesday, March 5, 2013

Songas hawezi kugoma kuuzia umeme Tanesco


KATIBU Mkuu wa wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi amesema Songas, (mwekezaji anayezalisha umeme na kuuzia Tanesco) hana uwezo wa kugoma kuliuzia shirika hilo umeme.

Kauli hiyo ilitokana na taarifa kwamba Tanesco limelemewa na mzigo wa madeni, kiasi cha kushindwa kujiendesha huku baadhi ya wawekezaji wakitishia kusitisha kuliuzia umeme.

Songas, ambayo taarifa mbalimbali zinasema inaidai Tanesco Sh 80 bilioni, ilitajwa na Maswi kwamba  nayo inadaiwa na serikali dola za Marekani 10.4 milioni, sawa na Sh16.64 bilioni.

“Songas hana ubavu kuzima mitambo maana siyo mmiliki pekee wa mitambo hiyo; serikali kupitia TPDC na Tanesco inamiliki asilimia 29 ya hisa za uwekezaji ukiachilia mbali anayeendesha mitambo kampuni ya Pan African,” alieleza Maswi. Alisema serikali itamlipa lakini itakata fedha zake inazomdai.

No comments:

Post a Comment