Monday, March 4, 2013

Tume kufuatilia anguko la mitihani ya Kidato cha Nne
Hivi karibuni Waziri mkuu Mizengo Pinda ameunda tume inayoongozwa na Profesa Sifuni Mchome, eti kutafuta suluhisho la matokeo mabaya ya mitihani ya kidato cha nne nchini.
Kumbukumbu zinaonesha utafiti wa aina hiyo umewahi kufanywa mwaka 2010, matokeo yake yaliwasilishwa serikalini na kuna mapendekezo ambayo yalitokana na utafiti huo, lakini hakuna hata moja lililotekelezwa.
Watanzania tujiulize, tume hizi mpaka lini? Fedha kiasi gani zinatumika kulipa wajumbe wa tume, kuiwezesha kutekeleza majukumu wanayopewa? Naamini fedha hizo zingetumika kutekeleza moja au baadhi ya mapendekezo yaliyowahi kutolewa katika tafiti lizowahi kufanywa, nchi ingepiga hatua kielimu.
Muda wa blablaa umepita, serikali na watendaji achene kuchezea fikra za wananchi tuliowapa dhamana badala yake tekelezeni majukumu yenu kwa dhamira safi ama sivyo, vizazi vijavyo vitawahukumu na pengine kuchapa viboko makaburi yenu.
Huu ni mtazamo wangu tu.

No comments:

Post a Comment