Thursday, February 28, 2013

UNAFAHAMU?
Wizi wa dawa serikalini ni changamoto kubwa kwa utekelezaji wenye ufanisi wa Bohari Kuu ya Dawa Tanzania (MSD)?
nitakuletea alichodokeza mkurugenzi wa MSD kuhusu hilo
 
Usiyoyajua kuhusu MSD
Je, unafahamu Bohari kuu ya Dawa Tanzania (MSD) hununua dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara  kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma ya afya nchini kutoka vyanzo gani?
Pata taarifa kama haufahamu;
Dawa: asilimia 80% huagizwa kutoka nje ya nchi
Vifaa tiba: asilimia 95% huagizwa kutoka nje ya nchi
Vitendanishi: asilimia 100% huagizwa kutoka nje ya nchi

Monday, February 25, 2013

hata mimi, Editha Majura nilikuwepo Mtwara; yaani we acha tu.
Nguli katika tasnia ya habari ndani ya Bongo na 'mji kasoro bahari' nao walikuwepo Mtwara.
Rahel na shost wake huyo, si unamfahamu eh, nao walikuwepo Mtwara.
hao ndiyo John na George Maratu bwana! ndani ya Mtwara

Sharon naye alikuwepo,
Hivi ndivyo Babo alivyopigwa risasi Bagamoyo
Gidalis Babo (18) Mbarbaig, anazungumza akishindwa kuzuia machozi kutengeneza njia mashavuni mwake, anasema mwishoni mwa mwaka jana, yeye na wafugaji wenzake wasiyopungua Kumi, walifatwa na jirani yao kwamba Ng’ombe wake Sita wameibwa.
Jirani yao huyo anayemiliki Ng’ombe 100, inaelezwa kuwa awali alikuta hiyo mifugo yake imewekwa kizuizini na Mzee Chamiwa, kwa kuwakuta wakinywa maji kwenye Bwawa alilotengeneza ndani ya himaya yake.
Babo anasema baada ya mazungumzo (kati yam Chamiwa na jirani yao) waliafikiana kesho yake jirani ya Babo akalipe faini (fedha ingawa haikulezwa kiasi gani) akaruhusiwa kuchukua mifugo yake.
Hatahivyo, Ngiombe walipofikishwa nyumbani na kuhesabiwa ikabainika Sita wamepungu. Ndipo Babo pamoja na wenzake wakakusanyika kuanza kazi ya kusaka Ngiombe waliopotea au ibiwa. Eneo la kwanza waliona vyema waanzie nyumbani kwa Chamiwa.
“Tukiwa nyumbani kwa Mzee Chamiwa hatukuona mtu, tukazunguka zunguka  nyumba ndipo tukaona eneo lililotifuliwa, tulipochimba tukaona vichwa viwili vya Ng’ombe na ngozi zake, kisha tukamuona mtoto wa huyo mzee tukaanza kumuhoji walipo Ng’ombe wengine,” anaeleza Babo.
Anasema wakati wakiendelea kumuhoji, akatokea Mzee Chamiwa akiwa amepakiwa kwenye pikipiki almaarufu bodaboda. Alipoteremka, akawafata huku akiwa na kitu mkononi, inadaiwa Babo hakujua kuwa ilikuwa bunduki, alifikiri ni aina ya fimbo za kujihami.
Anasema aliruka na kushika hiyo fimbo (bunduki) mfugaji mwenzao akawaambia kuwa hiyo ni bunduki, wakimbie lakini kabla hafanya lolote, alishtukia akipigwa na vitu sehemu tofauti za mwili wake na akaanguka, akapoteza fahamu.
Gidufana Gafifem, jamaa yake Babo anasema, wenzao wengi walikimbia baada ya kushuhudia ndugu yao damu zikimtoka kwa wingi.
Anasema aliyempiga risasi Babo alikuwa ndani ya nyumba ya Mzee Chamiwa na kwamba walipoona Babo ameanguka na wenzake wengi wamekimbia, nao wakachomoka kama mishare ndani ya nyumba na kukimbia.
Anasema bunduki aliyokuwanayo Chamiwa walifanikiwa kumnyang’anya. Pamoja na Mzee Chamiwa, silaha hiyo na mabaki ya Ng’ombe wawili waliyoyapata  waliyawasilisha kituo cha polisi Miono.
Hatahivyo, mpaka wakati wakizungumzia tukio hili wilayani Bagamoyo, mtuhumiwa alikuwa uraiani. Wanasema hakuna anayefahamu amepata vipi dhamana kwakuwa hawafahamu kama kuna kesi ilifikishwa mahakamani au la kwakuwa ndugu na jamaa wanahangaika kuuguza ndugu yao Babo.
Usikose awamu ijayo ya taarifa hii, itahusu anachoeleza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi

Friday, February 22, 2013




 Naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii, (Mb. Rufiji - CCM) akizungumza kwenye kongamano lililoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini, (NHIF) ambao umemalizika muda si mrefu mjini Mtwara.
 
 
 
 
 

MFUMO mpya wa utendaji kazi utakaoweza kuunganisha mamlaka zote zinazofanya kazi katika huduma ya afya, unafanyiwa kazi na serikali kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa ujumla, hususan katika upatikanaji dawa zenye ubora katika vituo mbalimbali vya afya.

Naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii, ameyazungumza hayo muda dakika chache zilizopita wakati wa kongamano la Nane la wahariri, wanahabari na wadau mbalimbali wa sekta ya afya nchini, ambalo huandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Wanahabari wamefanya tafiti katika wilaya 26 nchini, kuibua yanayojiri juu ya matumizi ya fedha zitokanazo na michango ya mifuko ya NHIF na mfuko wa afya wa jamii, (CHF).

Kila siku ya Jumatano, nitakuwa naleta taarifa za tafiti zilizowasilishwa kwenye kongamano hili, kuanzia wiki ijayo. Usikose na baadaye nakuletea  ‘maneno’ ya mtoto wa kibarbaig wilayani Bagamoyo akieleza alivyopigwa risasi tatu na kupooza.

 

Sunday, February 17, 2013

eti tuisheni kwenye shule za Engilish Medium?
Jamani, hawa walimu wanaofundisha katika shule za msingi za kulipia, a.k.a English Medium, alafu wanatumia mbinu mbalimbali kushawishi wazazi wawalipe fedha ‘vichochoroni’ kwa madai ya kuwafundisha tuisheni watoto wanaakili timamu kweli?
Hivi katika hili wa kulaumiwa ni mwalimu anayedai alipwe ili atumie mbinu za kibindoni za kufundishia kwa mtoto wako au ni mzazi ambaye bila shaka kilichoijaza nafsi yake ni roho ya ubinafsi na uchoyo?
Bila shaka wote wawili mnastahili kulaumiwa, kulaaniwa na hamfai katika jamii kwa maana mnanyong’onyeza elimu nchini.
Mnanyong’onyeza uwezo wa kitaaluma walionao watoto wengine ambao wazazi wao mbali na kumudu kuwasomesha katika shule hizo, hata kama wana pesa za kutoa kununua tuisheni, hawaoni sababu ya kufanya hivyo huku wakilipa milioni kadhaa kila mwaka.

aliyeiro Watanzania, bora awaonee huruma wwakomboe kwa maana hali imefikia ukomo wa ubaya.


GIDALIS Babo (18), bado yupo hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo. Jumatano alipelekwa MOI, ikaamuriwa abaki alipo mpaka Machi 1, mwaka huu atakapopelekwa kutolewa vyuma mkononi.
Taarifa ya alivyojeruhiwa na athari alizopata zimetolewa rasmi:

-         Pingili ya uti wa mgongo imetobolewa kwa risasi, atakuwa kilema milele; hataweza kusimama wala kutembea.
-          Risasi ya mgongoni haikutolewa kwa maelezo kwanga ilivyokaa ingetolewa ingesababisha madhara makubwa zaidi
-          Mkononi pia risasi bado ipo, haijafahamika kama itatolewa au nayo ataendelea kuishi nayo mwilini.

Naandaa taarifa ya Gidalis kuhusu alivyopatwa na mkasa huu, usikose kufuatilia.

 
Kila ninapofikiria huwa nashindwa kuelewa wanaoiba fedha za umma wa watanzania na kuzificha kwenye nchi za wenzao, tena zilizoendelea wana roho ya aina gani; ebu angalia Godoro linalotumiwa na mama, dada, shangazi na wadogo zetu wanapotekeleza jukumu lao la 'kuujaza ulimwengu' kwenye kituo cha afya kilichopo Dodoma, wilayani Maswa.

Kituo kinamilikiwa na serikali, mbali na magodoro kuchakaa hakuna shuka. mgonjwa akiwa na shuka inakuwa nafuu asipokuwa nalo inakuwa kama inavyoonekana.

Friday, February 15, 2013


Serikali yakunjua makucha dhidi ya migogoro baina ya wananchi na wawekezaji
KUTOKA kushoto, Mkurugenzi wa Viwanda vya kuongeza thamani wa Shirika la Maendeleo nchini (NDC), Shannel Mvungi na Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Dk. Anacleti Kashuliza wakikabidhiana mikataba ya ushirikiano.
Leo Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) limetangaza kuunganisha nguvu na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kuwafumbua macho na kuzindua akili za wananchi waone na kutumia fursa zinazokuwepo kwenye maeneo yenye miradi inayoendeshwa na NDC nchini.
Wameanzia kwenye mradi wa uchimbaji wa Makaa ya Mawe ya Mchuchuma na Chuma cha Liganga wilayani Ludewa. Watatoa mafunzo ya kutambua fursa na kuzitumia kukuza uchumi, kuwawezesha kupata mitaji na kuainisha, kuendeleza maeneo huru ya kufanyia biashara.
Kwetu kunamsemo usemao, “Empisi ekanyampila eibale, eti nolwo’otagamba  wakaulila.” Usemi huu unaendana na vurugu za wananchi wakipinga kusafirishwa gesi kutoka huko kupelekwa Dar es Salaam kwani baada ya hayo,  inaashiria serikali imehisi kitu na sasa imeanza kuchukua hatua.



Gidalis Babo (18) Mbarbaig aliyejeruhiwa kwa risasi mwishoni mwa mwaka jana, mkoani Pwani, wilayani Bagamoyo eneo la Miono amepooza. Inadaiwa Daktari wa wodi namba Sita, hataki aendelee kuwapo hospitalini hapo kwa maelezo kuwa amepona.
Ndugu zake wanasema, “Ingawa tunaamini afya yake haijaruhusu aondolewe hospitali, ndugu zetu walio kijijini alivyo huku mtuhumiwa wakipishana naye uraiani, Wabarbaig tunawafahamu wataleta maafa hata kama wanafahamu hawatakuwa salama mikononi mwa polisi,” anaeleza Gidufana Gafifem.
OCD alipopelekewa taarifa zinazoelezwa na ndugu za Babo, akashuhudiwa akimpigia simu DC (Ahmed Kipozi), “Yule kijana aliyejeruhiwa kwa risasi kwenye mgogoro wa wakulima na wafugaji, wakati akitolewa muhimbili hali yake ikawa mbaya ikabidi awekwe hospitali ya wilaya, sasa nasikia wanataka aondoke hospitalini…, tunaomba msaada wako maana hali ya usalama inaweza kuwa shakanai.”
DC alipoulizwa akasema analishughulikia, akasikika akizungumza na mganga wa wilaya (DMO), ikaafikiwa abaki. (taarifa zote hizi zimepatikana Jumamosi, wiki iliyopita.)
Lakini Jumatatu ya wiki hii mmoja wa ndugu wa Babo akapiga simu akisema, Daktari wa wodi amesisitiza mgonjwa tumuondoe akisema,
“Niliwaambia leo mwisho kuwa wodi hii, badala ya kumtoa mnaniletea vyombo vya habari? hata kama uongozi umeniambia abaki, lazima atoke ina maana hawajui kuwa mimi ndiye daktari? Mking’ang’ania namuandikia arudishwe Muhimbili  tuone kama nako mtang’ang’ania.” (sauti ya Daktari akizungumza hayo imerekodiwa)
Je, amebaki wodini?, amehamishiwa muhimbili? Au amefukuzwa? Naendelea kufuatilia; usikose kufungua Double Cleopa kila unapoingia mtanadaoni.