Sunday, February 17, 2013



GIDALIS Babo (18), bado yupo hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo. Jumatano alipelekwa MOI, ikaamuriwa abaki alipo mpaka Machi 1, mwaka huu atakapopelekwa kutolewa vyuma mkononi.
Taarifa ya alivyojeruhiwa na athari alizopata zimetolewa rasmi:

-         Pingili ya uti wa mgongo imetobolewa kwa risasi, atakuwa kilema milele; hataweza kusimama wala kutembea.
-          Risasi ya mgongoni haikutolewa kwa maelezo kwanga ilivyokaa ingetolewa ingesababisha madhara makubwa zaidi
-          Mkononi pia risasi bado ipo, haijafahamika kama itatolewa au nayo ataendelea kuishi nayo mwilini.

Naandaa taarifa ya Gidalis kuhusu alivyopatwa na mkasa huu, usikose kufuatilia.

 

No comments:

Post a Comment