Sunday, February 17, 2013

eti tuisheni kwenye shule za Engilish Medium?
Jamani, hawa walimu wanaofundisha katika shule za msingi za kulipia, a.k.a English Medium, alafu wanatumia mbinu mbalimbali kushawishi wazazi wawalipe fedha ‘vichochoroni’ kwa madai ya kuwafundisha tuisheni watoto wanaakili timamu kweli?
Hivi katika hili wa kulaumiwa ni mwalimu anayedai alipwe ili atumie mbinu za kibindoni za kufundishia kwa mtoto wako au ni mzazi ambaye bila shaka kilichoijaza nafsi yake ni roho ya ubinafsi na uchoyo?
Bila shaka wote wawili mnastahili kulaumiwa, kulaaniwa na hamfai katika jamii kwa maana mnanyong’onyeza elimu nchini.
Mnanyong’onyeza uwezo wa kitaaluma walionao watoto wengine ambao wazazi wao mbali na kumudu kuwasomesha katika shule hizo, hata kama wana pesa za kutoa kununua tuisheni, hawaoni sababu ya kufanya hivyo huku wakilipa milioni kadhaa kila mwaka.

aliyeiro Watanzania, bora awaonee huruma wwakomboe kwa maana hali imefikia ukomo wa ubaya.

No comments:

Post a Comment