Friday, February 15, 2013




Gidalis Babo (18) Mbarbaig aliyejeruhiwa kwa risasi mwishoni mwa mwaka jana, mkoani Pwani, wilayani Bagamoyo eneo la Miono amepooza. Inadaiwa Daktari wa wodi namba Sita, hataki aendelee kuwapo hospitalini hapo kwa maelezo kuwa amepona.
Ndugu zake wanasema, “Ingawa tunaamini afya yake haijaruhusu aondolewe hospitali, ndugu zetu walio kijijini alivyo huku mtuhumiwa wakipishana naye uraiani, Wabarbaig tunawafahamu wataleta maafa hata kama wanafahamu hawatakuwa salama mikononi mwa polisi,” anaeleza Gidufana Gafifem.
OCD alipopelekewa taarifa zinazoelezwa na ndugu za Babo, akashuhudiwa akimpigia simu DC (Ahmed Kipozi), “Yule kijana aliyejeruhiwa kwa risasi kwenye mgogoro wa wakulima na wafugaji, wakati akitolewa muhimbili hali yake ikawa mbaya ikabidi awekwe hospitali ya wilaya, sasa nasikia wanataka aondoke hospitalini…, tunaomba msaada wako maana hali ya usalama inaweza kuwa shakanai.”
DC alipoulizwa akasema analishughulikia, akasikika akizungumza na mganga wa wilaya (DMO), ikaafikiwa abaki. (taarifa zote hizi zimepatikana Jumamosi, wiki iliyopita.)
Lakini Jumatatu ya wiki hii mmoja wa ndugu wa Babo akapiga simu akisema, Daktari wa wodi amesisitiza mgonjwa tumuondoe akisema,
“Niliwaambia leo mwisho kuwa wodi hii, badala ya kumtoa mnaniletea vyombo vya habari? hata kama uongozi umeniambia abaki, lazima atoke ina maana hawajui kuwa mimi ndiye daktari? Mking’ang’ania namuandikia arudishwe Muhimbili  tuone kama nako mtang’ang’ania.” (sauti ya Daktari akizungumza hayo imerekodiwa)
Je, amebaki wodini?, amehamishiwa muhimbili? Au amefukuzwa? Naendelea kufuatilia; usikose kufungua Double Cleopa kila unapoingia mtanadaoni.

No comments:

Post a Comment