Naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii, (Mb. Rufiji - CCM) akizungumza kwenye kongamano lililoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini, (NHIF) ambao umemalizika muda si mrefu mjini Mtwara.
MFUMO mpya wa utendaji kazi utakaoweza kuunganisha
mamlaka zote zinazofanya kazi katika huduma ya afya, unafanyiwa kazi na
serikali kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa ujumla, hususan katika
upatikanaji dawa zenye ubora katika vituo mbalimbali vya afya.
Naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii, ameyazungumza
hayo muda dakika chache zilizopita wakati wa kongamano la Nane la wahariri,
wanahabari na wadau mbalimbali wa sekta ya afya nchini, ambalo huandaliwa na
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Wanahabari wamefanya tafiti katika wilaya 26 nchini,
kuibua yanayojiri juu ya matumizi ya fedha zitokanazo na michango ya mifuko ya
NHIF na mfuko wa afya wa jamii, (CHF).
Kila
siku ya Jumatano, nitakuwa naleta taarifa za tafiti
zilizowasilishwa kwenye kongamano hili, kuanzia wiki ijayo. Usikose na baadaye
nakuletea ‘maneno’ ya mtoto wa kibarbaig
wilayani Bagamoyo akieleza alivyopigwa risasi tatu na kupooza.
No comments:
Post a Comment