Friday, February 22, 2013




 Naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii, (Mb. Rufiji - CCM) akizungumza kwenye kongamano lililoandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini, (NHIF) ambao umemalizika muda si mrefu mjini Mtwara.
 
 
 
 
 

MFUMO mpya wa utendaji kazi utakaoweza kuunganisha mamlaka zote zinazofanya kazi katika huduma ya afya, unafanyiwa kazi na serikali kwa lengo la kuboresha huduma za afya kwa ujumla, hususan katika upatikanaji dawa zenye ubora katika vituo mbalimbali vya afya.

Naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii, ameyazungumza hayo muda dakika chache zilizopita wakati wa kongamano la Nane la wahariri, wanahabari na wadau mbalimbali wa sekta ya afya nchini, ambalo huandaliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Wanahabari wamefanya tafiti katika wilaya 26 nchini, kuibua yanayojiri juu ya matumizi ya fedha zitokanazo na michango ya mifuko ya NHIF na mfuko wa afya wa jamii, (CHF).

Kila siku ya Jumatano, nitakuwa naleta taarifa za tafiti zilizowasilishwa kwenye kongamano hili, kuanzia wiki ijayo. Usikose na baadaye nakuletea  ‘maneno’ ya mtoto wa kibarbaig wilayani Bagamoyo akieleza alivyopigwa risasi tatu na kupooza.

 

No comments:

Post a Comment