Monday, February 25, 2013

Hivi ndivyo Babo alivyopigwa risasi Bagamoyo
Gidalis Babo (18) Mbarbaig, anazungumza akishindwa kuzuia machozi kutengeneza njia mashavuni mwake, anasema mwishoni mwa mwaka jana, yeye na wafugaji wenzake wasiyopungua Kumi, walifatwa na jirani yao kwamba Ng’ombe wake Sita wameibwa.
Jirani yao huyo anayemiliki Ng’ombe 100, inaelezwa kuwa awali alikuta hiyo mifugo yake imewekwa kizuizini na Mzee Chamiwa, kwa kuwakuta wakinywa maji kwenye Bwawa alilotengeneza ndani ya himaya yake.
Babo anasema baada ya mazungumzo (kati yam Chamiwa na jirani yao) waliafikiana kesho yake jirani ya Babo akalipe faini (fedha ingawa haikulezwa kiasi gani) akaruhusiwa kuchukua mifugo yake.
Hatahivyo, Ngiombe walipofikishwa nyumbani na kuhesabiwa ikabainika Sita wamepungu. Ndipo Babo pamoja na wenzake wakakusanyika kuanza kazi ya kusaka Ngiombe waliopotea au ibiwa. Eneo la kwanza waliona vyema waanzie nyumbani kwa Chamiwa.
“Tukiwa nyumbani kwa Mzee Chamiwa hatukuona mtu, tukazunguka zunguka  nyumba ndipo tukaona eneo lililotifuliwa, tulipochimba tukaona vichwa viwili vya Ng’ombe na ngozi zake, kisha tukamuona mtoto wa huyo mzee tukaanza kumuhoji walipo Ng’ombe wengine,” anaeleza Babo.
Anasema wakati wakiendelea kumuhoji, akatokea Mzee Chamiwa akiwa amepakiwa kwenye pikipiki almaarufu bodaboda. Alipoteremka, akawafata huku akiwa na kitu mkononi, inadaiwa Babo hakujua kuwa ilikuwa bunduki, alifikiri ni aina ya fimbo za kujihami.
Anasema aliruka na kushika hiyo fimbo (bunduki) mfugaji mwenzao akawaambia kuwa hiyo ni bunduki, wakimbie lakini kabla hafanya lolote, alishtukia akipigwa na vitu sehemu tofauti za mwili wake na akaanguka, akapoteza fahamu.
Gidufana Gafifem, jamaa yake Babo anasema, wenzao wengi walikimbia baada ya kushuhudia ndugu yao damu zikimtoka kwa wingi.
Anasema aliyempiga risasi Babo alikuwa ndani ya nyumba ya Mzee Chamiwa na kwamba walipoona Babo ameanguka na wenzake wengi wamekimbia, nao wakachomoka kama mishare ndani ya nyumba na kukimbia.
Anasema bunduki aliyokuwanayo Chamiwa walifanikiwa kumnyang’anya. Pamoja na Mzee Chamiwa, silaha hiyo na mabaki ya Ng’ombe wawili waliyoyapata  waliyawasilisha kituo cha polisi Miono.
Hatahivyo, mpaka wakati wakizungumzia tukio hili wilayani Bagamoyo, mtuhumiwa alikuwa uraiani. Wanasema hakuna anayefahamu amepata vipi dhamana kwakuwa hawafahamu kama kuna kesi ilifikishwa mahakamani au la kwakuwa ndugu na jamaa wanahangaika kuuguza ndugu yao Babo.
Usikose awamu ijayo ya taarifa hii, itahusu anachoeleza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi

No comments:

Post a Comment