Sunday, February 17, 2013

Kila ninapofikiria huwa nashindwa kuelewa wanaoiba fedha za umma wa watanzania na kuzificha kwenye nchi za wenzao, tena zilizoendelea wana roho ya aina gani; ebu angalia Godoro linalotumiwa na mama, dada, shangazi na wadogo zetu wanapotekeleza jukumu lao la 'kuujaza ulimwengu' kwenye kituo cha afya kilichopo Dodoma, wilayani Maswa.

Kituo kinamilikiwa na serikali, mbali na magodoro kuchakaa hakuna shuka. mgonjwa akiwa na shuka inakuwa nafuu asipokuwa nalo inakuwa kama inavyoonekana.

No comments:

Post a Comment