Friday, February 15, 2013


Serikali yakunjua makucha dhidi ya migogoro baina ya wananchi na wawekezaji
KUTOKA kushoto, Mkurugenzi wa Viwanda vya kuongeza thamani wa Shirika la Maendeleo nchini (NDC), Shannel Mvungi na Katibu Mtendaji wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Dk. Anacleti Kashuliza wakikabidhiana mikataba ya ushirikiano.
Leo Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) limetangaza kuunganisha nguvu na Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) kuwafumbua macho na kuzindua akili za wananchi waone na kutumia fursa zinazokuwepo kwenye maeneo yenye miradi inayoendeshwa na NDC nchini.
Wameanzia kwenye mradi wa uchimbaji wa Makaa ya Mawe ya Mchuchuma na Chuma cha Liganga wilayani Ludewa. Watatoa mafunzo ya kutambua fursa na kuzitumia kukuza uchumi, kuwawezesha kupata mitaji na kuainisha, kuendeleza maeneo huru ya kufanyia biashara.
Kwetu kunamsemo usemao, “Empisi ekanyampila eibale, eti nolwo’otagamba  wakaulila.” Usemi huu unaendana na vurugu za wananchi wakipinga kusafirishwa gesi kutoka huko kupelekwa Dar es Salaam kwani baada ya hayo,  inaashiria serikali imehisi kitu na sasa imeanza kuchukua hatua.

No comments:

Post a Comment