Friday, March 22, 2013

WANAHABARI TUREJEE MAADILI


UANDISHI ni taaluma kama  nyingine. Ina maadili na kanuni zake. Moja ya maadili ambayo mwandishi anatakiwa kuzingatia ni  kutoingiza ushabiki katika kazi.
Miaka iliyopita, Abdallah Majura akitangaza moja ya  mechi, kati ya Simba na Yanga alishindwa kuficha mapenzi yake kwa timu anayoipenda. Aliibua gumzo mitaani.
Kisa cha kuibuka gumzo si kwamba jamii haifahamu kuwa ana chaguo lake, la hasha! bali maadili yalikuwa yakizingatia kwa kiwango cha kushtusha, ikitokea mtu akaonekana ameyakiuka.
hata Jane Mihanji alitekeleza rasmi hatua ya kuingia kwenye ulingo wa siasa, wengi walionekana kushtushwa kidogo kwa sababu awali maadili ya uandishi yalizuia kabisa kujihusisha na masuala yote ya aina hiyo.
Ingawa ni wazi kwamba kwasababu wanahabari ni wanadamu,  wana utashi na maono yao binafsi, wanatakiwa kuyaweka kando pindi wanapofanya kazi. Bila shaka hii ni kwa maslahi yao binafsi na jamii kwa ujumla.
Siamini kuwa waasisi wa misingi na maadili ya uanahabari hawakuwa na akili walipoamua hivyo.
Ukitafakari kwa kina utabaini kuwa walikuwa makini na wenye kuona mbali sana.
Maadili ya kazi hii yasipozingatiwa na chombo cha habari au mwanahabari mmojammoja dunia inaweza kugeuka mahala pasipo salama.
Leo tujiulize, tunafanya kazi zetu kwa kusimamia misingi ya uandishi wa habari? Bila shaka jibu ni hapana.
Kwanini? Hapa kila mmoja ana jawabu lake lakini kimsingi ninachoona ni njaa.
Ukihomi kwanini gazeti lenye hadhi ya kitaifa litoe toleo huku ukurasa wa mbele ukiwa umefunikwa na tangazo la Kampuni au biashara fulani, jibu litabaki kuwa ni njaa ya pesa.
 
Ukihoji kwa nini gazeti linalomilikiwa na chama cha siasa, litoe habari kuu ambayo kwa 100% ni kwa maslahi ya chama husika, jibu linabaki kwamba tatizo ni njaa, ya madaraka au fedha.
Jambo la kushangaza ni kwamba, vyombo hivyo vinaongozwa na wanataaluma waliobobea, wenye sifa na uzoefu wa kutosha. sasa kwanini hali iwe hivi? Jibu ni lile lile; njaa.
Kuna haja ya kubadili mwelekeo kitaaluma, misingi ya uandishi wa habari ni maadili. Naamini kila mtu anayeitwa mwanahabari anaifahamu sina haja ya kuitaja.
 

 

 

 

No comments:

Post a Comment