UANDISHI
ni taaluma kama nyingine. Ina maadili na kanuni zake. Moja ya
maadili ambayo mwandishi anatakiwa kuzingatia ni kutoingiza ushabiki
katika kazi.
Miaka iliyopita, Abdallah Majura akitangaza moja ya mechi, kati ya Simba na
Yanga alishindwa kuficha mapenzi yake kwa timu anayoipenda. Aliibua gumzo mitaani.
Kisa cha kuibuka gumzo si kwamba jamii haifahamu kuwa ana chaguo lake, la hasha! bali maadili yalikuwa yakizingatia kwa kiwango cha kushtusha, ikitokea mtu akaonekana ameyakiuka.
hata Jane Mihanji alitekeleza rasmi hatua ya kuingia kwenye ulingo wa siasa, wengi walionekana kushtushwa kidogo kwa sababu awali maadili ya uandishi yalizuia kabisa kujihusisha na masuala yote ya aina hiyo.
Ingawa ni wazi kwamba kwasababu wanahabari ni wanadamu, wana utashi na maono yao
binafsi, wanatakiwa kuyaweka kando pindi wanapofanya kazi. Bila shaka hii ni kwa maslahi yao
binafsi na jamii kwa ujumla.
Siamini kuwa
waasisi wa misingi na maadili ya uanahabari hawakuwa na akili walipoamua hivyo.
Ukitafakari kwa kina utabaini kuwa walikuwa makini na wenye kuona mbali sana.
Maadili ya
kazi hii yasipozingatiwa na chombo cha habari au mwanahabari
mmojammoja dunia inaweza kugeuka mahala pasipo salama.
Leo tujiulize,
tunafanya kazi zetu kwa kusimamia misingi ya uandishi wa habari? Bila shaka
jibu ni hapana.
Kwanini? Hapa kila mmoja ana jawabu lake lakini kimsingi
ninachoona ni njaa.
Ukihomi kwanini
gazeti lenye hadhi ya kitaifa litoe toleo huku ukurasa wa mbele ukiwa
umefunikwa na tangazo la Kampuni au biashara fulani, jibu litabaki kuwa ni njaa
ya pesa.
Ukihoji kwa
nini gazeti linalomilikiwa na chama cha siasa, litoe habari kuu
ambayo kwa 100% ni kwa maslahi ya chama husika, jibu linabaki kwamba tatizo ni njaa, ya madaraka au fedha.
Jambo la kushangaza ni kwamba, vyombo hivyo vinaongozwa na wanataaluma waliobobea, wenye sifa na
uzoefu wa kutosha. sasa kwanini hali iwe hivi? Jibu ni lile lile;
njaa.
Kuna haja
ya kubadili mwelekeo kitaaluma, misingi ya uandishi wa habari
ni maadili. Naamini kila mtu anayeitwa mwanahabari anaifahamu sina
haja ya kuitaja.
No comments:
Post a Comment