Hayo yamejiri wakati akitaka kuonesha kuwa alichozungumza Tundu Lissu
(Mb)kwamba msemaji wa kambi ya upinzani hakugusia kesi, wala ushahidi
uliyotolewa katika kesi inayoendelea
mahakamani hakikuwa kweli.
Selukamba alikaririwa akisema, “Madai kwamba kambi
ya upinzani haikuzungumzia kesi iliyo mahakamani
si yakweli, ukingalia ukurasa wa nne,” ikasikika mingong’ono iliyoashiria kutoridhishwa na alichokuwa akizungumza; mara sautiikasikika
ikisema, “fuck you!”
Haya yanafanyika ndani ya Bunge, huku vyombo vya habari
vikirusha matangazo ya moja kwa moja. inasikitisha, inatia
aibu taifa.
Tanzania tutafaulu katika lipi? Elimu zii,
kilimo zii, uchumi zii, michezo zii, ni kipi chenye manufaa kwa maisha yetu ya
kila siku, tutakachofanya vizuri duniani? Kiongozi ni kioo cha jamii hivyo
tunapowatazama viongozi bungeni ndipo tunapopata taswira ya jamii yetu.
Tujikague
tumekwama wapi, tuchukue hatua la sivyo, tutaishia kulalama tu na mwisho wa
siku hakuna la maana litakalotendeka zaidi ya kutukanana; wengine aina ya
maisha yao ni matusi tosha unapomuingiza kwenye ulingo wa matusi inakuwa sawa
na kumsukuma mlevi.
No comments:
Post a Comment