Wednesday, April 17, 2013

PETER SELUKAMBA!!!!!!!


Leo Peter Selukamba (Mbunge Kigoma mjini (CCM) amefunga kazi ya matumizi ya matusi bungeni, baada ya kutoa tusi zito kuliko waliomtangulia.

Hayo yamejiri wakati akitaka kuonesha kuwa alichozungumza Tundu Lissu (Mb)kwamba msemaji wa kambi ya upinzani hakugusia kesi, wala ushahidi uliyotolewa katika kesi inayoendelea  mahakamani hakikuwa kweli.

Selukamba alikaririwa akisema, “Madai kwamba kambi ya  upinzani haikuzungumzia kesi iliyo mahakamani si yakweli, ukingalia ukurasa wa nne,” ikasikika mingong’ono iliyoashiria kutoridhishwa na alichokuwa akizungumza; mara sautiikasikika ikisema, “fuck you!”

Haya yanafanyika ndani ya Bunge, huku vyombo vya habari vikirusha matangazo ya moja kwa moja. inasikitisha, inatia aibu taifa.

Tanzania tutafaulu katika lipi? Elimu zii, kilimo zii, uchumi zii, michezo zii, ni kipi chenye manufaa kwa maisha yetu ya kila siku, tutakachofanya vizuri duniani? Kiongozi ni kioo cha jamii hivyo tunapowatazama viongozi bungeni ndipo tunapopata taswira ya jamii yetu.

Tujikague tumekwama wapi, tuchukue hatua la sivyo, tutaishia kulalama tu na mwisho wa siku hakuna la maana litakalotendeka zaidi ya kutukanana; wengine aina ya maisha yao ni matusi tosha unapomuingiza kwenye ulingo wa matusi inakuwa sawa na kumsukuma mlevi.

No comments:

Post a Comment