Friday, April 12, 2013

MABARAZA YA KATIBA MPYA YA TZ AU CHAMA FULANI?


Mwenzenu nimejionea maajabu kwenye uchaguzi wa wajumbe wa mabaraza ya Katiba ngazi za wilaya.

Jaji Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya Katiba Tanzania, Joseph Warioba
Miongoni mwa wagombea wa nafasi hiyo, waliofika mbele ya Kamati ya maendeleo ya Kata ya Tabata inayoongozwa na diwani mwanamama Mtumwa, ni pamoja na wakili wa kujitegemea.

Bila shaka, alikusudia kutumia taaluma yake kuchangia mchakato wa taifa kujikwamua na changamoto nyingi zinazolikabili. ha! kwani Kamati ilijali uanasheria?!  Hakuchaguliwa bwana!
Waliochaguliwa kwa haraka ilibainika kuwa sifa ya kwanza na ya msingi ni wana chama kimoja tu. Kila mtu sasa anahoji ikiwa kinachokwenda kufanywa ni kupitia rasimu ya Katiba chama hicho au ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

No comments:

Post a Comment