Friday, April 5, 2013

KIMENUKA KWA JERRY SLAA!

                          Rajaba Mbarouk Mohammed
Hivi umeona ujenzi unaoendelea kwenye ‘round-about’ kadhaa katikati ya jiji la Dar es Salaam? kwa mfano unapokuwa barabara ya uhuru kuelekea mtaa wa kongo? Lile eneo limeenezwa makatuni, vinyago, limesakafiwa na kuchorwa michoro mfano wa bahari? Kama umeona ni vizuri ikiwa bado, nitapiga picha kisha niiweke uelewe ninachoeleza.

Sasa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) imeshtukia dili. Mwenyekiti wa LAAC, Rajaba Mbarouk Mohammed leo amesema wakiwa ziarani wilayani humo wameshtushwa na ujenzi huo. Mbali na kushutushwa na ubunifu huo ambao bado haijaeleweka unalenga nini, wamesikia gharama zake zinatolewa na ‘wafadhili’

Hoja ni kwamba, wafadhili hao wanafaidikaje? LAAC inawasiwasi kwamba, hiyo inaweza kuwa mbinu ya ama kukwepa kulipia mabango ya matangazo ya biashara; lakini kwakuwa manispaa hiyo imegoma kufika mbele ya kamati hiyo kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali likiwamo hilo, kama kamati hiyo ilivyoagiza, yote hayo bado ni kitendawili.

No comments:

Post a Comment