Rajaba Mbarouk Mohammed
Hivi umeona ujenzi unaoendelea kwenye ‘round-about’
kadhaa katikati ya jiji la Dar es Salaam? kwa mfano unapokuwa barabara ya uhuru
kuelekea mtaa wa kongo? Lile eneo limeenezwa makatuni, vinyago, limesakafiwa na
kuchorwa michoro mfano wa bahari? Kama umeona ni vizuri ikiwa bado, nitapiga picha
kisha niiweke uelewe ninachoeleza.
Sasa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali
(LAAC) imeshtukia dili. Mwenyekiti wa LAAC, Rajaba Mbarouk
Mohammed leo amesema wakiwa ziarani wilayani humo wameshtushwa na ujenzi huo. Mbali
na kushutushwa na ubunifu huo ambao bado haijaeleweka unalenga nini, wamesikia
gharama zake zinatolewa na ‘wafadhili’
Hoja ni kwamba, wafadhili hao wanafaidikaje?
LAAC inawasiwasi kwamba, hiyo inaweza kuwa mbinu ya ama kukwepa kulipia mabango
ya matangazo ya biashara; lakini kwakuwa manispaa hiyo imegoma kufika mbele ya
kamati hiyo kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali likiwamo hilo, kama kamati
hiyo ilivyoagiza, yote hayo bado ni kitendawili.
No comments:
Post a Comment