Wednesday, April 17, 2013

CHIKU ABWAO NAYE ATEMA CHECHE BUNGENI


Chiku Abwao, viti maalumu (Chadema) anasema matusi, vurugu bungeni na kutikiswa kwa amani nchini kunatokana kunatokana na Chama Cha Mapinduzi, ambacho ni chama cha siasa kikongwe kuliko vyote nchini, kutosikiliza vilio vya wananchi.

Anasema wabunge wa kambi ya upinzani wanapoingia bungeni na kuwasilisha kiliio cha wapigakura wake, anazomewa, anabezwa na kuonekana hasemi lolote; matokeo yake nao wanajibu mapigo ndiyo maana bunge linaonekana kama ilivyo sasa.

(tofauti na zamani, sasa bunge limegubikwa na matumizi ya lugha za kukera na matusi hali inayosababisha kudhalilisha wahusika na taifa kwa ujumla)

Abwao anasema matukio ya watu kung’olewa kucha, meno na kujeruhiwa kwa namna tofauti kwanini yanawapata wanaoonekana kukosoa utendaji wa serikali?

Anasema hali hiyo ikihusishwa na hali iliyopo bungeni ambapo watu wanakosa uvumilivu hadharani kiasi cha hicho, inatia shaka watu hao wanapokuwa nje ya hadhara wanaweza kutenda mangapi.

No comments:

Post a Comment