Friday, October 25, 2013

PPF IMETUMIA 3 BIL KUSOMESHA YATIMA WA WANACHAMA WAKE



Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio, akizungumza kwenye mkutano na Kamati ya Bunge ya masuala ya UKIMWI
Mkurugenzi wa Mfuko wa Akiba wa PPF, William Erio akizungumza na Kamati ya Kudumu ya Bunge, ya masuala ya UKIMWI na dawa za kulevya leo, katika makao makuu ya mfuko huo jijini Dar es Salaam.

Mfuko huo kwa miaka 10 umeelezwa kutumia Sh. Bilioni 3 kusomesha watoto waliofiwa na wazazi wao, ambao walikuwa wananchama wake na tangu Januari mpaka Juni mwaka huu, Sh milioni 615 zimetumika kusomesha yatima 1,151; kuanzia chekechea hadi kidato cha nne.
Mwakani, mfuko huo utaongeza ufadhili huo kwa kusomesha watoto wa aina hiyo mpaka kidato cha sita.
Erio anaomba Kamati hiyo katika shughuli zake iongeze na kazi ya udhibiti wa dawa za kulevya, kwakuwa anaamini sasa ni janga la kitaifa hususan kwa watu walio katika rika la ujana.

No comments:

Post a Comment